Baada ya kushindwa 'ku-do' jamaa aua sita kuonyesha yeye ni kidume!

Mwanaume mwenye asili ya Russia ameua watu sita kwa kuwapiga risasi katika eneo lake la kazi baada  ya kuelezwa kushindwa kuwajibika kitandani(kimapenzi)!

Dmitry Vinogradov mwanaume mwenye umri wa miaka 30amewatuhumu jamaa hao sita kuwa walimshawishi mpenzi wake Anna Kaznikova amuache kabla ya kuwaua.

Akijieleza mbele ya polisi  Dmitry anasema alifanya kitendo hicho ili kudhihirisha kwa mpenzi wake kuwa yeye ni mwanaume kamili na anaweza kufanya lolote ukiachia mbali udhaifu wake wa kushindwa kuwajibika vyema kitandani!

Wakati wa mapumziko ya weekend tulienda  Suzdal.,hapo mimi na Anna tulifanya mapenzi kwa mara ya kwanza lakini haikuwa na mafanikio kwa sababu ya aibu zangu na kushindwa kumtimizia kimapenzi kitu kilichowahi kunitokea kabla..baada ya hapo Anna alini bwaga na kukata mawasiliano na mimi" alisema Dmitry

Hiyo ndio sababu iliyofanya Dmitry kufanya ukatili wa kuua watu wasio na hatia ili kuonyesha uanaume wake..mmmh mapenzi haya!

0 Maoni:

Toa Maoni