Isabella Mpanda afunguka kuhusu muziki, Scorpion girls na ugomvi wake na Kabula

Isabella Mpanda au Miss Ruvuma asiyechuja kama anavyojiita amefunguka leo kupitia Hatua Tatu ya Times fm Kuhusu swala la kuingia katika muziki,mahusiano yake na mwanamuziki mwenzake Luteni Kalama na ugomvi wake na Jini Kabula.
Bella katika studio za Times
Baada ya kipindi tukapata picha
Mie na Bella

Akizungumzia kuhusu muziki,Bella anasema ameamua kuingia rasmi kwenye muziki na kashatoa single yake kama solo artist inayoitwa 'Jikubali mwenyewe' ambayo inapatikana kwenye audio na video.Kutoa singo kama solo artist haimaanishi kuwa katoka kwenye kundi lao la muziki Scorpion Girls ila tu ni katika kukuza muziki wake zaidi huku Kalama akiwa ni meneja wake.Anasema yeye na Luteni kalama wana mipango mingi ikiwa kufunga ndoa na kutengeneza familia.

Pia akizungumzia Scorpion girls,anasema kundi hilo lipo na linaundwa na wasanii wengi tu akiwemo yeye mwenyewe,Kabula,Jacky Pentizel,Aunt Lulu, Sajenti na wengine.

Akizungumzia maneno yaliyozagaa kuhusu kugombana na Kabula na  kumtupia vitu nje,Bella anasema ni kweli waligombana sababu ikiwa ni  Kabula kumtukana matusi mazito baada ya Bella kumsifia mwana Scorpion mwenzao Jacky Pentizel kwa kununua gari.Ila anasema hajawahi kumfukuza wala kumtupia vitu nje Kabula maana hawaishi pamoja yeye anakaa na familia yake.

1 comment:

  1. MAMU KITOSI UMEPENDEZA MASHAALLAH NATAMANI RAMADHANI ISIISHE ILI UWENDELEE KUVAA HIVI.

    ReplyDelete