Washiriki wapata mshtuko baada ya Emerald kuaga jumba la BBA

Baada ya kuingia katika jumba la Big brother Ijumaa iliyopita,washiriki sita ambao ni feki (Emerald housemates) hatimaye wameaga jumba hilo usiku wa jana huku wakiacha mshtuko wa washiriki wa kweli .Lengo la kuwaingiza washiriki hao sita feki ilikuwa ni kuwachanganya housemates na kuwashawishi kuwa wao ni washiriki wa kweli kitu walichokimudu kwa kuteka baadhi ya akili za housemates.



Baada ya kumaliza presentation ya Task waliyopewa na Big  brother,washiriki wote waliitwa sehemu moja na kupongezwa.Kilichofata Emerald housemates waliitwa Diary room na waliobaki waliwashiwa screen na Big kupasuwa bomu kuwa Emerald walikuwa ni feki kitu kilichowaacha washiriki wakiduwaa kasoro Annabell na Angelo ambao walitia mashaka mpaka dakika ya mwisho. Kilichofatia baada ya hapo ni gumzo tu kwa washiriki wakizungumzia mchezo waliochezewa na kukumbuka baadhi ya matukio ya Emerald housemates na kupata picha kuwa kweli walikuwa feki!

Sulu kutoka Zambia,Elikem wa Ghana pamoja na Anabell kutoka nchini Kenya wamekuwa nominated wiki hii huku washiriki kutoka Tanzania Feza na Nando wakiendelea kuwa salama kwa mara nyingine tena.

0 Maoni:

Toa Maoni