Polisi nchini Uchina imetangaza kuwa itatoa zawadi kwa yeyote atakayetoa habari zitakazowasaidia kumkamata mama mmoja ambaye anashukiwa kumng'oa macho mvulana mwenye umri wa miaka sita.
![]() |
| Mtoto aliyeng'olewa akiwa hospitali |
Mvulana huyo anasemekana alikwenda kucheza na watoto wengine lakini wazazi wake walimpata baadaye huku macho yake yote yakiwa yamengolewa huku akivuja damu. Polisi walipata macho ya mvulana huyo karibu na eneo la tuko.
Idara ya polisi nchini humo imetoa zawadi ya zaidi ya dola elfu kumi na sita kwa yeyote atakayetoa habari, kuhusu aliyehusika na shambulio hilo.
Wazazi wa mtoto huyo wanasemekana kuwa wakulima. Mamake amesema mtoto huyo aliwaambia kuwa wakati alipokuwa akitembea alishambuliwa na mama mmoja ambaye hakumfahamu.
Uchunguz wa awali umebainisha kuwa sehemu ya mboni au Cornea kwa Kiingereza ilikuwa imengolewa, na hivyo kuashiria ulanguzi wa viungo vya kinadamu.
Hata hivyo polisi wanasema hawajatambua chanzo cha shambulio hilo.Mvulana huyo kwa sasa anaendelea kupata matibabu hospitalini.

Hii hatari habari kwa wanaokimbia nchi yao na kwenda ng'ambo
ReplyDeleteInauma sana
ReplyDelete