Babu wa miaka 92 ajisevia binti mbichii!

Kweli ng'ombe hazeeki maini! usemi huu unathibitishwa na Mzee wa miaka 92 Muslai Mohamed kutoka nchini Iraq ambae amefunga ndoa na binti wa miaka 22 baada ya kufiwa na mke wake miaka mitatu iliyopita.

"Nilibaki peke yangu baada ya mke wangu kufarki.hamna mtu aliyeniliwaza kwa chochote na hatimaye Mungu kaniletea mke na nnafuraha"amesema Muslai.
Muna al-Jabouri, mke wake mpya nae akafunguka"Nilikubali kuolewa nae nilipoona picha yake nikaona ndio rizki yangu"

Cheki video fupi ya tukio.       

0 Maoni:

Toa Maoni