Dibibi awachana wanaoingilia ndoa yake na Jack Pentzel

Mume wa nyota wa tasnia ya filamu nchini Jack "Kauthar"Dibibi ,Gadner Dibibi amefunguka la moyoni akisema mke wake huyo ni msafi wa tabia na anampenda kwa dhati ya moyo.

Dibibi amesema tokea ameingia kwenye ndoa na nyota huyo wa filamu amekuwa anafurahia maisha na mapenzi anayopata kutoka kwake akitumikia ndoa yake kama mke anayejua majukumu na wajibu wake.

Amesema mke wake ni mwenye tabia ya kupendeza,muaminifu na tokea wameingia kwenye ndoa hajawahi kukutana naa tabia yoyote mbaya ama chafu kutoka kwa Jack ambaye kwasasa anafahamika kama Kauthar.

Dibibi amefunguka zaidi akisema amekuwa karibu na mke wake na wakishirikiana katika mambo mengi kiasi hata password kila mmoja anafahamu ya mwenzake,iwe ya bank au hata kwenye mitandao ya kijamii ya facebook na twitter,na hata simu zao kila mmoja yuko huru na simu ya mwenzake jambo ambalo linaongeza uaminifu kwao.
Amesema watu hawapaswi kumfikiria tofauti mke wake kwakuwa amebadilika na mwenye kujua wajibu wa mke,huku akisema mambo ya nyuma ya mke wake hataki kuyaafuatilia kwakuwa hata yeye akifuatiliwa ya nyuma anaweza kuwa sio msafi.

Akiwafunga watu midomo Dibibi amesema maisha yake na Jack yanakwenda safi na wanafurahia ndoa yao,akiwataka watu kuacha maneno ya kufuatilia ndoa yao na kusema vibaya,kikubwa ni wao wanapendana kwa dhati ya mioyo yao.

0 Maoni:

Toa Maoni