Tiwa Savage na meneja wake mahaba live..bonge la harusi kufanyika Dubai!

 
Baada ya kufunga ndoa ya kimila iliyofanyika Lagos November 23 mwaka jana,staa wa muziki kutoka nchini Nigeria mwanadada mrembo Tiwa Savage na mume ambaye ni meneja wake pia Tee Billz wanatarajiwa kudondosha  bonge la white wedding tarehe 26 April Dubai.


Wawili hawa ambao waligeuka gumzo baada ya kuonyesha mahaba live walipo-share kiss jukwaani kwenye tamasha la Gidi Culture lililofanyika March 02 Lagos wamesogeza mbele harusi hiyo ambayo mwanzo ilipangwa kufanyika February...habari za chini chini zinasema itakuwa ni harusi ya kufunga mwaka kwa mastaa! Kila la heri kwao.

Cheki picha za jinsi walivyojiachia jukwaani.

0 Maoni:

Toa Maoni