Baada mchezaji wa timu ya Barcelona, Dani Alves kula ndizi
aliyorushiwa na mashabiiki uwanjani, kitendo chake kimechukuliwa kama
kitendo cha kishujaa na kimeanzisha harakati mpya za kupinga ubaguzi wa
rangi kwa mtindo wa kula ndizi.
Mastaa mbalimbali wametumia mitandao ya kijamii kupost picha wakila ndizi na maelezo ya kupinga ubaguzi wa rangi.
“Straggling to sleep after tonight’s game…this banana might help #Weallmonkeys #Notoracism” ameandika Drogba katika picha aliyopost akiwa na ndizi huku akijaribu kusinzia.
“Say No to Racism” ameandika Davido na kupost picha akiwa anakula ndizi.
Mastaa wengine wa wa rangi zote duniani wameendelea kupost picha za aina hiyo kupinga vitendo vya kibaguzi.
Baada ya mechi ambayo aliyotupiwa ndizi, Alves alisema:
“Tumeumia na haya maumivu kwa muda, unatakiwa kuyachukua na dozi ya heshima. Hatutaweza kubadili vitu kirahisi. Kama hauipi umuhimu, hawafanikishi malengo yao. Sijui alikuwa nani, lakini namshukuru yeyote aliyetupa ndizi, ilinipa nguvu ya kupiga crosses mbili ambazo zilipelekea kufunga goli.”
Mtu aliyerusha ndizi alifahamika na amefungiwa kuingia uwanjani hapo katika maisha yake yote.
Habari kwa hisani ya tovuti ya Times fm, bofya www.timesfm.co.tz kuingia.
Mastaa mbalimbali wametumia mitandao ya kijamii kupost picha wakila ndizi na maelezo ya kupinga ubaguzi wa rangi.
“Straggling to sleep after tonight’s game…this banana might help #Weallmonkeys #Notoracism” ameandika Drogba katika picha aliyopost akiwa na ndizi huku akijaribu kusinzia.
“Say No to Racism” ameandika Davido na kupost picha akiwa anakula ndizi.
Mastaa wengine wa wa rangi zote duniani wameendelea kupost picha za aina hiyo kupinga vitendo vya kibaguzi.
Baada ya mechi ambayo aliyotupiwa ndizi, Alves alisema:
“Tumeumia na haya maumivu kwa muda, unatakiwa kuyachukua na dozi ya heshima. Hatutaweza kubadili vitu kirahisi. Kama hauipi umuhimu, hawafanikishi malengo yao. Sijui alikuwa nani, lakini namshukuru yeyote aliyetupa ndizi, ilinipa nguvu ya kupiga crosses mbili ambazo zilipelekea kufunga goli.”
Mtu aliyerusha ndizi alifahamika na amefungiwa kuingia uwanjani hapo katika maisha yake yote.
Habari kwa hisani ya tovuti ya Times fm, bofya www.timesfm.co.tz kuingia.


0 Maoni:
Toa Maoni