Miss IFM 2014 Kufunguka ndani ya The Playlist ya Times Fm Jumapili hii

Kipindi cha The Playlist cha 100.5 Times Fm kinachoongozwa na Omary Tambwe aka Lil Ommy, Jumapili hii kitamdondosha mrembo aliyeshinda taji la Miss IFM 2014, Lilian Timoth.

Akiwa kama mrembo ambaye amepata nafasi ya kuingia kwenye orodha ya celebs wa Tanzania katika tasnia ya ulimbwende, Lilian atazicheza nyimbo tano kali anazozipenda zaidi huku akijibu maswali ya kichokozi yanayomhusu.

The Playlist inakuwa hewani kila Jumapili saa kumi kamili jioni hadi saa kumi na moja kamili jioni kupitia 100.5 Times Fm.

Fuatilia The Playlist kwenye mitandao ya kijamii, Twitter na Instagram @LilOmmy @TimesfmTZ @lilytimoth

0 Maoni:

Toa Maoni