Ni zamu ya Times fm sasa,ukurasa wake wa facebook wahalalishwa.

Baada ya hivi karibuni mwanamuziki Diamond Platnumz kutambulika rasmi katika mtandao wa facebook baada ya account yake ya facebook kuwa verified,sasa ni zamu ya Times fm.



100.5 Times FM inaendelea kufanya vizuri katika upande wa vipindi na mitandao ya kijamii katika kuwahusisha wasikilizaji na jamii kwa ujumla habari, elimu na burudani na wakati huu ukarasa wake wa Facebook umehalalishwa na Kampuni ya Facebook (Verified).

Ukurasa huo wa Facebook (Times FM TZ) ambao unapewa sapoti na wasikilizaji wa Times FM umefanikiwa kupata alama ya tick ya blue kama ishara ya kuitambua Times Fm kuwa mmiliki halali wa ukurasa huo.

Mitandao mingine ya kijamii ya Times Fm inaendelea kufanya vizuri pia, Twitter @timesfmtz, Instagram @timesfmtz na Facebook Times Fm Tz.

0 Maoni:

Toa Maoni