Denrele asema hutokewa na Goldie akimlalamikia kutochukua hatua kwa aliyesababisha kifo chake!



Ni zaidi ya mwaka sasa tangu aliyekuwa mshiriki wa BBA na mwanamuziki kutoka Nigeria Suzan Harvey 'Goldie' alipofariki dunia ( Febr 14,2013) huku akiacha mipango mingi ikipotea ikiwemo ule wa kuanzisha Reality show ya televisheni ambayo kwa pamoja na rafiki yake mpenzi Denrele Edun  wangeonekana.

Akifanya interview na Sahara Tv, Denrele amefunguka kuwa Goldie amekuwa akimtokea ndotoni mpaka sasa akimlalamikia kuwa anajua aliyemuua lakini hafanyi chochote kuhusu hilo kitu kilichofanya story hii itokee hapa ndani ya MamuAfrica blog;

" Naendelea kumuona kwenye ndoto zangu na ananiambia unajua aliyesababisha kifo changu ..aliyeniua na hufanyi chochote kuhusu hilo... hili sidanganyi.  Unajua haya mambo wengi hatuamini maana si vitu vya kawaida.'' Alifunguka Denrele.

Cheki mahojiano hayo hapa chini.

                    

0 Maoni:

Toa Maoni