Timu hizo zilimaliza dakika 90 bila kufungana na dakika 30 za nyongeza nazo hazikumpata mbabe mpaka kwenye mikwaju ya matuta ambako Italy walikosa mkwaju mmoja.
Leonardo Bonucci wa Italy alikosa mkwaju wa penati uliopaa juu ya lango na Jesus Navas wa Hispania akapata mkwaju wake uliowapeleka Hispania fainali na sasa watacheza dhidi ya wenyeji Brazil hapo Jumapili kwenye uwanja wa Maracana.
Raha ya kwenda fainali kwa wachezaji wa Hispania
Jesus Navas akitumbukiza mkwaju ulioipeleka Hispania fainali



0 Maoni:
Toa Maoni