Benteke awasilisha ombi la kutaka kuondoka Villa



Aston Villa wamethibitisha kuwa Christian Benteke amewasilisha maombi ya kutaka kuondoka kwenye timu hiyo na wamekubali kumuachia kama itatokea offer ya kumchukua.

Benteke alitua Villa kwa dau la paundi milioni 7 akitokea Genk na amefunga mabao 19 kwenye ligi kuu ya Uingereza.

Benteke anahusishwa kutakiwa na Atletico Madrid, Arsenal, Chelsea, Liverpool, Manchester City na Tottenham Hotspur.

0 Maoni:

Toa Maoni