Nilipata nafasi ya kutembelea maeneo mbalimbali Bagamoyo mwanzoni mwa mwaka huu na zifuatazo ni baadhi ya picha katika maeneo tofauti niliyopita.
![]() |
| Hapa panaitwa Caravan Serai ni sehemu ambayo waarabu waliokuwa wanafanya biashara ya utumwa wanafikia kwa ajili ya mapumziko kwa ndani humo. |
![]() |
| Hapa panaitwa Ngome Kongwe |
![]() |
| Hayo ni makaburi ya baadhi ya viongozi wa kiarabu wa enzi za utumwa. Wageni mbalimbali hufika hapa kutembea na kujionea. |
![]() |
| Mimi pia nilipata nafasi ya kujionea.Makaburi ya viongozi yamewekewa minara na kila kaburi linatofautiana urefu wa mnara kutokana na cheo cha aliyefariki. |
![]() |
| Hapa nilikuwa naoneshwa Bandari iliyokuwepo kwa mbele kidogo pamoja na mashamba ya mikoko |
![]() |
| Hili ni shamba la mamba ambapo Mamba hufugwa na wageni hupita kujionea |
![]() |
| Baadae nilipita baharini kupunga upepo yakhee! |















0 Maoni:
Toa Maoni