Oprah na vijimambo vya ndoa

Mmoja kati ya wanawake maarufu na tajiri duniani Oprah Winfrey amefunguka kuwa hana mpango wa kuolewa kabisa licha ya kupata msukumo kutoka kwa rafiki yake aliyeolewa hivi karibuni mwanamuziki Tina Turner.
Oprah na Tina wamekuwa marafiki kwa miaka sasa na alipohudhuriwa harusi ya Tina iliyofanyika July akatambua mambo ya ndoa sio kwa upande wake.''Nafikiri inaweza kushangaza nilifikia tena nilipokuwa kwenye harusi ya Tina maana aliniambia 'unatakiwa ufanye hivi' nikafikiria tofauti yake nini'' alisema Oprah

Oprah pia kafafanua kuwa hawezi kuwa mke kwa sababu kuna majukumu mengi ambayo anahisi hayuko tayari kukabiliana nayo.

Kuna uasemi unasema 'mwanamke hata uwe na hela nyingi kiasi gani bila kuwa na mume ni sawa na bure'...eti kweli?

0 Maoni:

Toa Maoni