Dr. Cheni afungukia uhusiano wake na Lulu..

Ukaribu uliokuwepo kati ya msanii wa Filamu Tanzania Dr. Cheni na mwigizaji mwenzake Elizabeth Michael a.k.a Lulu umeibua maswali mengi sana kwa watu huku kukiwa na tetesi kuwa wawili hao ni wapenzi.
Dr. Cheni katika studio ya Times fm
Hatimaye leo kupitia Kipindi cha Hatua Tatu cha  Times fm Dr. Cheni amefungukia uhusiano wake na Lulu na kusema amekuwa akisikia maneno mengi mtaani watu wakimtuhumu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Lulu lakini ukweli ni kwamba hakuna kinachoendelea katika yao zaidi ya kuwa mstari wa mbele kumsaidia alipopatwa na matatizo na kuwekwa rumande kama binadamu.

Team Hatua Tatu Mie,Mkisi na Dr Cheni studio leo
 Akiendelea kufunguka Cheni amesema anawashangaa watu wanaozusha mbona alishawahi kumsaidia msanii mwenzake Cloud alipopata matatizo na alikuwa mstari wa mbele kwenda polisi,kumpelekea chakula n.k lakini hakuna aliyesema lolote  kwamba atakuwa na mahusiano na dada wa Cloud au nini iweje kwa Lulu wazungumze!

Habari nyingine kutoka kwa Dr. Cheni ni kuwa anatarajia kutoka na filamu mpya itakayoitwa Nimekubali kuolewa huku kwenye cover ya mbele itaonekana picha yake mwenyewe akiwa katinga shela na chini ya picha hiyo kuna maandishi kwa hiyari yangu, kwa hiyo ni  Nimekubali kuolewa kwa hiyari yangu..kaa tayari kwa burudani.

0 Maoni:

Toa Maoni