Bata za kupewa na sugarmami zamponza na kujitoa uhai!

Jamani wale wanaopenda maisha ya luxury bila kufanya kazi soma hii story ya kusikitisha ya kijana mdogo wa miaka 22 aliyejitoa uhai kisa kutoswa na sugamami!


Michael Jaja kijana mwenye miaka 22 amejiua baada ya kutemwa na mpenzi wake aliyemzidi umri na aliyekuwa akimuwezesha kimaisha (sugamami) mwenye umri wa miaka 48.

Kijana huyu aliwahi kuzawadia gari la aina ya Toyota Corolla na safari za kwenda nchini China na Dubai zilizolipiwa kila kitu. Pia walikuwa wakiishi pamoja kwenye jumba la kifahari la mume wa mwanamke huyo huku mambo yakionekana kwenda shwari mpaka mwanamke huyo alipozua janga hilo kwa kutaka waachane sababu ikiwa ni kwamba mumewe anarejea kutoka ulaya alipokwenda.

Kama kawaida habari hii haikupokelewa vyema na Michael ambaye alitishia kujiua kama itatokea kuachana na mwanamama huyo na kwenda mbali zaidi baada ya kujiua kweli na kabla ya hayo inasemekana ugomvi mkubwa sana ulitokea baina yao.


Inasemekana kwa mujibu wa Michael hakutaka kushuhudia au watu kumuona akirudi kwenye maisha yake ya kimaskini baada ya bata alizozoeshwa!

Jamani fanyeni kazi kwa bidii acheni kutegemea mali za kuhongwa ambazo mwisho wa siku zinawagharimu na kufanya maamuzi ya ajabu kama ya kijana hapo!

0 Maoni:

Toa Maoni