Kama wewe ni shabiki na mpenzi wa muziki mzuri wa live band basi Valentine hii itakuwa tamu sana kwako Banana
Zorro, Nuruel na wengine wanaounda bendi ya B. Band, siku ya Valentine
(Ijumaa, February 14), kuanzia saa tatu kamili hadi saa sita kamili
iweke kwenye ratiba yako muhimu ili uisikilize bendi hiyo ikiimba na
kupiga Live kupitia kipindi
Hatua Tatu cha 100.5 Times Fm.
 |
| Banana Zoro,Stara Thomas,Edson Mkisi Jr na mie studio katika Kipindi cha Hatua tatu |
Bendi hiyo itawapa mashabiki burudani kwa muda mfupi
itakaokuwa ndani ya studio za Times Fm, na kisha burudani hiyo itahamia
‘Club East 24’ iliyoko maeneo ya Mikocheni, Dar es Salaam kuanzia saa
mbili kamili usiku. Kiingilio kitakuwa shilingi 15,000 kwa mtu mmoja na
shilingi 25,000 kwa watu wawili (double).
Katika show hiyo iliyoandaliwa na B band kwa kushirikiana na kipindi cha Hatua Tatu,
watakuwepo wasanii wengine wakali akiwemo Stara Thomas, Grace Matata,
Maunda Zorro na mwana hip hop Kala Jeremiah aliyeshirikishwa kwenye wimbo mpya watakaouzindua kesho '
you are not alone'.
Zawadi kwa watakaopendeza zitatolewa na watakaofika watapata nafasi ya kuwaimbilia live wapenzi wao huku wakipiwa ala za muziki na B.Band.
MUHIMU: Kutakuwa na comlimentary zitakazotolewa katika kipindi cha Hatua Tatu kesho so niazime tu sikio lako waweza kujipatia yako.
0 Maoni:
Toa Maoni