Bibi wa miaka 97 aonekana akijifua gym..vijana wenye nguvu mpo?

Mwanamke mwenye umri mkubwa wa miaka 97 amewashangaza wengi baada ya video yake inayoonyesha yuko gym akipiga push-up na mazoezi mengine ya viungo kuonekana katika mtandao wa Instagram.


Akiwa anafahamika kwa jina moja tu Edna,ameonekana mara kadhaa kwenye video alizoweka mwalimu wake wa mazoezi Antony Mackey na kusema 'Edna anasema siri yake ya kuwa na afya nzuri ni mazoezi na anawashauri wengine wasikubali kuwa dhaifu'

Huu ni kama ujumbe kwa vijana wenye nguvu lakini kufanya mazoezi kwao ni kama adhabu lol!

Bibi akijifua.

0 Maoni:

Toa Maoni