Khloe Kardashian afata nyendo za dada yake Kim, sasa ajiweka kwa French Montana!

Khloe na French Montana
Akiwa amejipatia umaarufu pamoja na familia yake kupitia kipindi cha telesheni kinachoonyesha maisha yao kinachojulikana kama Keeping up with the Kardashians,mwanadada Khloe Kardashian inasemekana amezama kimahaba kwa rapper French Montana baada ya kuonekana katupia cheni shingoni ya gold yenye neno la kiarabu lenye tafsiri ya jina halisi la rapa huyo.

E News wamethibitisha kuwa maana ya neno la kiarabu lililopo kwenye cheni ya Khloe ni 'Karim' ambalo jina halisi la French Montana((Karim Kharbouch)) ambaye anatokea nchini Morrocco.


Hivi karibuni wawili hao wamekuwa na ukaribu mkubwa na wameonekana wakijirusha pamoja sehemu za starehe, wakitoka pamoja kupata chakula, wamekuwa wakisafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine n.k kitu kilichoibua tetesi kuwa ni wapenzi.

0 Maoni:

Toa Maoni