Kweli nabii hakubaliki kwao..Bieber azomewa kwao baada ya kushinda tuzo!

Tunaweza kuiita hii kuwa nabii hakubaliki kwao kwa asilimia zote. Jumapili, March 30 zilitolewa tuzo za Juno nchini Canada na mwimbaji ambaye ni raia wa nchi hiyo anaekubalika na wengi duniani alionekana kutopokelewa vizuri baada ya kutajwa kushinda tuzo.


Justin Bieber alitajwa kushinda tuzo ya ‘Fan Choice’ kwa mara ya nne katika tuzo hizo za nyumbani kwao Canada, lakini baada ya kutajwa watu walisikika wakizomea huku wengine wakishangilia.

Hata hivyo, mwimbaji huyo hakuwepo ukumbini hapo na hivyo tuzo yake kuchukuliwa kwa niaba yake. Baadae Justin alitweet kuonesha furaha yake kwa kushinda tuzo hizo.
“We won #JUNOFanChoice for the 4th year in a row! Love to all my biliebers. Thank u. love u (sic).”  Ilisomeka tweet ya Justin Bieber.

0 Maoni:

Toa Maoni