Wiki moja baada ya kushinda tuzo ya mitindo ya CFDA kama ‘Fashion Icon of the Year’, Rihanna ametajwa pia katika tuzo za Guys Choice Awards kama ‘Most Desirable Woman’.
Tofauti na ilivyokuwa kwenye CFDA alipozua balaa kwa vazi lake, Rihanna alipanda jukwaani kupokea tuzo hiyo akiwa amevaa vazi la heshima.
Rihanna alikabithiwa tuzo na mchekeshaji wa Marekani Kavin Hart ambaye alipomuona aliweka utani kama kawaida yake, “Ni wanaume wangapi wamekasirika kuwa hayuko mtupu?”
“Sawa, namaanisha, asanteni kwa kunipigia kura kushinda tuzo hii nikiwa na umri wa miaka 26 kwa sababu wote tunafahamu inaenda chini zaidi kutoka hapa. Lakini hii ni tuzo ya ucheshi, niappreciate.” Alisema Rihanna.
“Sawa, namaanisha, asanteni kwa kunipigia kura kushinda tuzo hii nikiwa na umri wa miaka 26 kwa sababu wote tunafahamu inaenda chini zaidi kutoka hapa. Lakini hii ni tuzo ya ucheshi, niappreciate.” Alisema Rihanna.
Habari kwa hisani ya tovuti ya Times fm tz.




0 Maoni:
Toa Maoni